STAA wa mduara Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amedhihirisha kuwa ni
sikio la kufa baada ya kusema yeye ni miongoni mwa wanawake wanaojua
kuchuna mabuzi.
Kauli hiyo imechochea vigezo vya kumfanya Shilole aonekane hasikii
kwani wiki kadhaa zilizopita mchungaji wa kanisa moja lililopo Ubungo,
jijini Dar ambaye hakujulikana jina lake, alimtaka kuishi katika sura ya
kumpendeza Mungu lakini inaonekana amempuuza.
Akizungumza na Risasi Mchanganyiko juzi, jijini Dar es Salaam,
Shilole alisema alitunga wimbo wa Nachuna Buzi kwa sababu anajua kuwa
wanawake wengi ni mafundi wa tabia hiyo akiwemo yeye mwenyewe!
Hata hivyo alisema japokuwa ana tabia hiyo lakini anatambua siyo
nzuri hivyo anawasihi wanawake wengine kuachana nayo kwani ipo siku
itawaingiza matatizoni.
Mbali na mchungaji huyo, juzi Jumapili, Mchungaji wa Kanisa la
Anglikana, Ukonga –Mazizini, Dar, Emmanuel Kapande alimtumia ujumbe wa
watoto wa Shule ya Jumapili (Sunday School) nyumbani kwake kwa lengo la
kuimba na kufanya maombi.
Ujumbe huo, ulimpelekea baraka ya maombi nyumbani kwake na kumshauri aishi katika mazingira yanayompendeza Mungu.
BOFYA HAPO CHINI KUUNGANA NASI KILA SIKU KWA HABARI MPYA ZENYE UTAMU
<<<<<BOFYA HAPA UPATE UPDATES KILA SIKU>>>